• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Musoma District Council
Musoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maji
      • Ujenzi
      • AFYA
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • AFYA
    • KILIMO
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayoanzishwa
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mikataba ya huduma kwa wateja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

MUSOMA DC: MIKATABA NANE YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA MUGANGO YASAINIWA.

Posted on: September 21st, 2018

Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kupitia kamati ya kituo cha Afya cha Mugango imesaini mikataba nane yenye thamani ya Shillingi Millioni 73,322,240 ambayo inajumisha kazi za ufyatuaji wa matofali na ujenzi wa majengo matano yanayotarajiwa kujengwa katika kituo cha Afya Mugango kilichopo Kata ya Mugango.

Zoezi hilo la utiaji saini wa mikataba ya ujenzi wa majengo ya upasuaji, kuhifadhia maiti, wodi ya kinamama, maabara, mtumishi na wafyatua matofali watatu lililohusisha kamati ya zahanati hiyo na wakandarasi (local fundi) limefanyika leo Ijumaa 21, Septemba 2018 katika ukumbi wa Zahanati hiyo uliopo Mugango.

Wakandarasi (local fundi) waliofanikiwa kupata kazi za ujenzi wa majengo hayo ni Ndg. Sylvanus A. Jairo atakayejenga jengo la kuhifadhia maiti, Ndg. Gideon Matto Egwaga atakayejenga jengo la wodi ya kinamama, Ndg. Hassan Ramadhan Magesa atakayejenga jengo la upasuaji, Ndg. Ernest Paschal Magige atakayejenga nyumba ya mtumishi na Yatanduka Co. Ltd itakayojenga jengo la maabara.

Sambamba na wakandarasi (local fundi) wa kujenga majengo hayo matano, waliofanikiwa kupata kazi ya kufyatua matofali yatakayotumika kwa ajili ujenzi huo ni Ndg. Paschal Nyagabona Anthon atakayefyatua matofali 6000, Ndg. Clifford James Nyamasagara atakayefyatua matofali 6000 na Ndg. Jumbula Macraud Rugola atayefyatua matofali 6500.

Ujenzi wa majengo hayo matano utakaotumia miezi minne tangu kuanza kwake 21, Septemba 2018 mpaka 19, January 2019 (kwa mujibu wa mkataba), utatumia njia ya kushirikisha wananchi katika kutekeleza mradi huo (force account).

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Afisa manunuzi msaidizi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma ambaye pia ni katibu wa kamati ya manunuzi ya ujenzi huo Ndg. Joseph Chana Maitarya  aliwataka mafundi  hao kuhakikisha wanajenga majengo yenye ubora sambamba na kumaliza ujenzi huo kwa wakati.

"Wengi walijitokeza kuomba kazi ya ujenzi huu, ila nyinyi ndio mmekidhi vigezo, kati yenu kuna walioomba kujenga majengo matatu, mawili na wengine yote matano, lakini tumeona ni vyema kila jengo lijengwe na fundi msimamizi wa ujenzi mmoja ili kuongeza ufanisi sambamba na kumaliza kazi kwa wakati" alisema Maitarya.

"Kwa maana hiyo naomba mafundi mliopata kazi hii muhakikishe majengo mnayajenga katika ubora wa hali ya juu utakaoendana na makubalino tuliokubaliana katika mikataba mliyosaini, pia hakikisheni ujenzi unakamilika kwa wakati" alisema Maitarya.

Akizungumza kwa niaba ya mafundi waliopata kazi ya ujenzi wa majengo hayo na ufyatuaji matofali Ndg. Jumbula Macraud Rugola aliishukuru kamati ya kituo cha Afya Mugango na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Ndg. John Lipesi Kayombo kwa kuendesha zoezi la kutafuta mafundi kwa uwazi na kwa weledi mkubwa sambamba na kupata kazi hizo.


Imetolewa na

Kitengo cha Habari na Uhusiano

Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

Matangazo

  • Fomu za kujiunga na Kidato cha Kwanza kwa Mwaka 2021 December 16, 2020
  • UPATIKANAJI WA TAARIFA ZA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI KWA NJIA YA MTANDAO September 20, 2018
  • ORODHA YA WATUMISHI WALIOHAMISHWA BAADA YA KUOMBEWA VIBALI VYA UHAMISHO NA MAKATIBU TAWALA WA MIKOA TANZANIA BARA - JANUARI_FEBRUARI 2018 March 27, 2018
  • Kushiriki Mbio za Mwenge September 04, 2018
  • Angalia Yote

Habari za sasa

  • MAAFISA ELIMU KATA WATAKIWA KUWA WABUNIFU NA KUENDANA NA KASI YA SERIKALI YA AWAMU YA TANO

    September 26, 2018
  • MUSOMA DC YASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA KUTOKOMEZA KICHAA CHA MBWA DUNIANI,BUTIAMA

    September 28, 2018
  • WANANCHI WAJITOLEA UJENZI WA KITUO CHA AFYA MUGANGO, UJENZI WAANZA

    October 01, 2018
  • MUSOMA DC: MIKATABA NANE YA UJENZI WA KITUO CHA AFYA MUGANGO YASAINIWA.

    September 21, 2018
  • Angalia Yote

Video

KAYOMBO AKEMEA VITENDO VYA KISHIRIKINA BUGOJI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • YALIYOJILI KAMATI YA FEDHA
  • Agreement on provision of health services by Japan Government

Tovuti mashuhuri

  • Necta
  • Utumishi
  • Ajira
  • Salary Slip

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Musoma Town opposite to Airport

    Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma

    Simu: 0282622163

    simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@musomadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa