Katika kuendelea kuimarisha mifumo ya mipango na utekelezaji wa shughuli za maendeleo, Halmashauri imeendesha mafunzo ya maandalizi ya Mpango Mkakati (SP) wa miaka mitano kwa kipindi cha 2026/2027–2030/2031, yaliyofanyika kuanzia tarehe 29 hadi 30 Januari, 2026.
Mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Charles Magoma, yamewakutanisha Wakuu wa Divisheni na Vitengo pamoja na watendaji mbalimbali wa Halmashauri kwa lengo la kujenga uelewa wa pamoja kuhusu mchakato wa maandalizi ya Mpango Mkakati, kubaini vipaumbele vya maendeleo, pamoja na kuweka misingi thabiti ya utekelezaji wa mipango ya muda wa kati na mrefu.
Kupitia mafunzo hayo, Halmashauri inalenga kuhakikisha Mpango Mkakati unaandaliwa kwa ufanisi, kwa kuzingatia miongozo ya kitaifa na mahitaji halisi ya wananchi.
Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Suguti - Kwikonero, Barabara ya Majita) | 31117 - MUSOMA.
Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma
Simu: 0282622163
simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@musomadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa