• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Musoma District Council
Musoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maji
      • Ujenzi
      • AFYA
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • AFYA
    • KILIMO
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayoanzishwa
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mikataba ya huduma kwa wateja
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

MKURUGENZI MTENDAJI (W) NDG. MSONGELA PALELA AFUNGA MAFUNZO YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KWA WENYEVITI WA VIJIJI – MUSOMA DC

Posted on: November 26th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji (W) wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma amefunga mafunzo maalumu yaliyofanyika tarehe 26 Novemba 2025 katika Ukumbi wa Jengo la Utawala – Afya, Kwikonero, yakilenga kuwajengea uwezo Wenyeviti wa Vijiji kuhusu utekelezaji wa Mkataba wa Lishe.

Mafunzo haya yamelenga kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji wa afua za lishe katika ngazi ya kijiji, na hivyo kuchochea ustawi wa afya ya jamii hususan watoto na mama wajawazito.

Mada zilizowasilishwa ni pamoja na:

* Dhana ya lishe, makundi ya vyakula na umuhimu wake

* Sheria ndogo za lishe

* Mwongozo wa Siku ya Afya na Lishe ya Kijiji (SALiKi)

* Zana ya upimaji na tathmini ya utekelezaji wa afua za lishe

* Mwongozo wa uchangiaji wa chakula shuleni (kiasi kinachohitajika kwa kila mwanafunzi na wajibu wa kijiji)

* Hamasa za lishe kupitia vikundi vya lishe, klabu, sanaa na mabango ya afya


Kupitia mafunzo haya, washiriki walikubaliana kutekeleza maazimio yafuatayo:

1. Kila kijiji kuanzisha daftari maalumu lenye orodha ya watoto wote walio chini ya miaka mitano.

2. Kila kijiji kuhakikisha maadhimisho ya Siku ya Afya na Lishe ya Kijiji (SALiKi) yanafanyika kwa ufanisi.

3. Kuendelea kuelimisha na kuhamasisha jamii kuhusu utoaji na uchangiaji wa chakula shuleni.

4. Kuhakikisha mafunzo na ujenzi wa uwezo kwa watekelezaji wa mkataba wa lishe, ikiwemo wenyeviti wa vijiji, yanaendelea kwa utaratibu endelevu.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji (W) amewaagiza viongozi hao kuanza mara moja kutoa hamasa juu ya kampeni ya Mwezi wa Afya na Lishe** itakayofanyika kuanzia 1 – 31 Desemba 2025.

Lengo kuu ni kuhakikisha kila mlengwa anapatiwa matone ya vitamini A pamoja na huduma nyingine muhimu za lishe.

Halmashauri ya Wilaya ya Musoma inaendelea kuimarisha juhudi za kuboresha afya na lishe ya wananchi wake kupitia ushirikiano na viongozi wa vijiji, wataalam, wadau na jamii kwa ujumla.

Matangazo

  • SIKU YA KUPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI OKTOBA 29, 2025 October 29, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA KATIKA WA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 October 20, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI 2025 October 03, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 14, 2022
  • Angalia Yote

Habari za sasa

  • MKURUGENZI MTENDAJI (W) NDG. MSONGELA PALELA AFUNGA MAFUNZO YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KWA WENYEVITI WA VIJIJI – MUSOMA DC

    November 26, 2025
  • ZIARA YA KAMATI YA MIKOPO ILIYOFANYIKA KISIWANI RUKUBA KATA YA ETARO.

    November 25, 2025
  • WANANCHI WA KIJIJI CHA KATARYO KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA LISHE KITAIFA 2025

    November 21, 2025
  • KILELE CHA MAADHIMISHO YA LISHE KITAIFA KATIKA KIJIJI CHA KATARYO KILICHOPO KATA YA TEGERUKA.

    November 21, 2025
  • Angalia Yote

Video

MANDHARI INAYOPATIKANA KISIWANI RUKUBA, KATA YA ETARO HALMASHAURI YA WILAYA YA MUSOMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal (PEPMIS)
  • Mfumo wa manunuzi (NeST)
  • PREM
  • PReMS
  • GMS
  • Mfumo wa kujisajiri kwa ajili ya bima ya afya (NHIF)

Tovuti mashuhuri

  • OWM - TAMISEMI
  • OR - UTUMISHI
  • NeST
  • NECTA
  • MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Suguti - Kwikonero, Barabara ya Majita) | 31117 - MUSOMA.

    Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma

    Simu: 0282622163

    simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@musomadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa