• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Musoma District Council
Musoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maji
      • Ujenzi
      • AFYA
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • AFYA
    • KILIMO
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayoanzishwa
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mikataba ya huduma kwa wateja
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

TIMU YA WATAALAM WA MKOA NA HALMASHAURI WAANZA ZIARA YA UFUATILIAJI WA MIRADI - MUSOMA DC

Posted on: January 14th, 2026

Timu ya Wataalam kutoka Mkoani leo tarehe 14 Januari, 2026 imeanza rasmi zoezi la ufuatiliaji na ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, zoezi lililoanza kwa kufanyika kwa kikao cha ufunguzi (Entrance Meeting).

Kikao hicho muhimu kiliwakutanisha Wataalam wa Mkoa pamoja na Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, ambapo pamoja na mambo mengine, wajumbe walijadili madhumuni ya ufuatiliaji wa miradi, upeo wa zoezi hilo, pamoja na kuweka mikakati ya ushirikiano katika kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa ufanisi, ubora na kwa kuzingatia thamani ya fedha.

Baada ya kikao hicho, Timu ya Wataalam wa Mkoa kwa kushirikiana na wataalam wa Halmashauri ilianza kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo tofauti ya wilaya hiyo. Katika ziara hizo, timu ilifanya ukaguzi wa kina kwa kujionea hatua za utekelezaji wa miradi, kukagua ubora wa kazi zinazofanyika, pamoja na kutathmini matumizi ya fedha ili kuhakikisha kuna thamani halisi ya fedha zilizotolewa (Value for Money).

Aidha, wataalam walipata fursa ya kuzungumza na wasimamizi wa miradi, wakandarasi pamoja na kamati za wananchi, ambapo walipokea maelezo ya utekelezaji wa miradi na kubaini changamoto mbalimbali zilizopo. Kupitia ukaguzi huo, Timu ya Wataalam wa Mkoa ilitoa ushauri wa kitaalam na maelekezo ya awali yenye lengo la kuboresha utekelezaji wa miradi, kuondoa mapungufu yaliyojitokeza na kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyokubalika.

Halmashauri ya Wilaya ya Musoma imeeleza kuendelea kushirikiana kikamilifu na Timu ya Wataalam wa Mkoa katika zoezi hilo, huku ikisisitiza dhamira yake ya kusimamia miradi ya maendeleo kwa kuzingatia misingi ya uwazi, uwajibikaji na tija, kwa lengo la kuboresha huduma za kijamii na kuharakisha maendeleo endelevu kwa wananchi.

Zoezi la ufuatiliaji wa miradi linaendelea kuwa sehemu muhimu ya kuhakikisha rasilimali za umma zinatumika ipasavyo na miradi inaleta matokeo chanya kwa wananchi wa Wilaya ya Musoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA KWANZA WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI November 27, 2025
  • SIKU YA KUPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI OKTOBA 29, 2025 October 29, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA KATIKA WA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 October 20, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI 2025 October 03, 2025
  • Angalia Yote

Habari za sasa

  • TIMU YA WATAALAM WA MKOA NA HALMASHAURI WAANZA ZIARA YA UFUATILIAJI WA MIRADI - MUSOMA DC

    January 14, 2026
  • DC CHIKOKA AHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU TATU KWA WAHESHIMIWA MADIWANI - AKEMEA MIGOGORO ISIYO NA TIJA.

    January 14, 2026
  • UFUATILIAJI WA MIRADI – MUSOMA DC

    January 14, 2026
  • MADIWANI WAPATA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO

    January 12, 2026
  • Angalia Yote

Video

MANDHARI INAYOPATIKANA KISIWANI RUKUBA, KATA YA ETARO HALMASHAURI YA WILAYA YA MUSOMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal (PEPMIS)
  • Mfumo wa manunuzi (NeST)
  • PREM
  • PReMS
  • GMS
  • Mfumo wa kujisajiri kwa ajili ya bima ya afya (NHIF)

Tovuti mashuhuri

  • OWM - TAMISEMI
  • OR - UTUMISHI
  • NeST
  • NECTA
  • MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Suguti - Kwikonero, Barabara ya Majita) | 31117 - MUSOMA.

    Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma

    Simu: 0282622163

    simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@musomadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa