• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Musoma District Council
Musoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maji
      • Ujenzi
      • AFYA
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • AFYA
    • KILIMO
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayoanzishwa
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mikataba ya huduma kwa wateja
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

VIFAA VYA KISASA KUONGEZA TIJA YA KILIMO CHA UMWAGILIAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUSOMA

Posted on: November 12th, 2025

Wakulima wadogo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Musoma wamepata neema baada ya kukabidhiwa jozi za mashine za umwagiiaji. Vifaa hivyo vimetolewa kama sehemu ya juhudi za serikali kuboresha kilimo cha umwagiliaji na kuongeza uzalishaji wa mazao ya bustani na mbogamboga.

Katika juhudi za kuboresha kilimo na kuhakikisha usalama wa chakula nchini, Wizara ya Kilimo kupitia Programu ya Mifumo Himilivu ya Chakula (Tanzania Food Systems Resilience Program - TFSRP), imekabidhi vifaa vya kisasa vya umwagiliaji kwa vikundi vya wakulima Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na pampu za maji, mipira ya umwagiliaji, mabomba, na vinyunyizi vya umwagiliaji ambavyo vitasaidia kuongeza ufanisi katika kilimo cha umwagiliaji hasa wakati wa vipindi vya ukame.

Makabidhiano ya vifaa hivyo yamefanyika Halmashauri ya Wilayaya Musoma, yakihusisha kata 21 zilizoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Mradi huo unalenga kuwawezesha wakulima wadogo kutumia teknolojia ya kisasa ya umwagiliaji ili kuongeza tija, kupunguza utegemezi wa mvua, na kuhakikisha uzalishaji wa mazao kwa mwaka mzima.

Baadhi ya wakulima walionufaika na mpango huo wameishukuru serikali kwa kuwapatia msaada huo, wakisema utaleta mabadiliko makubwa katika maisha yao wakibainisha kuwa kwa muda mrefu wamekuwa

wakitegemea mvua katika kilimo, hali iliyokuwa ikisababisha changamoto wakati wa vipindi vya ukame.

Kupitia vifaa hivi vya umwagiliaji, sasa watakuwa na uhakika wa mavuno na soko la mazao yao kwa mwaka mzima. Ugawaji wa vifaa hivyo ni sehemu ya juhudi endelevu za serikali za kuendeleza kilimo cha kisasa na cha umwagiliaji, kwa lengo la kuhakikisha Tanzania inakuwa na kilimo chenye tija, cha kibiashara, na chenye mchango mkubwa katika uchumi wa Taifa.

Matangazo

  • SIKU YA KUPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI OKTOBA 29, 2025 October 29, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA KATIKA WA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 October 20, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI 2025 October 03, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 14, 2022
  • Angalia Yote

Habari za sasa

  • WANANCHI WA KIJIJI CHA KATARYO KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA LISHE KITAIFA 2025

    November 21, 2025
  • KILELE CHA MAADHIMISHO YA LISHE KITAIFA KATIKA KIJIJI CHA KATARYO KILICHOPO KATA YA TEGERUKA.

    November 21, 2025
  • KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI YAANZA TATHMINI YA MAOMBI YA MIKOPO YA TSH 700 MILIONI KWA VIKUNDI VYA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    November 19, 2025
  • SALAMU ZA PONGEZI KUTEULIWA KUWA WAZIRI MKUU WA TANZANIA 2025 - 2030

    November 18, 2025
  • Angalia Yote

Video

KILELE CHA MAADHIMISHO YA LISHE KITAIFA YALIYOFANYIKA KIJIJI CHA KATARYO KATA YA TEGERUKA 2025
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal (PEPMIS)
  • Mfumo wa manunuzi (NeST)
  • PREM
  • PReMS
  • GMS
  • Mfumo wa kujisajiri kwa ajili ya bima ya afya (NHIF)

Tovuti mashuhuri

  • OWM - TAMISEMI
  • OR - UTUMISHI
  • NeST
  • NECTA
  • MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Suguti - Kwikonero, Barabara ya Majita) | 31117 - MUSOMA.

    Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma

    Simu: 0282622163

    simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@musomadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa