• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Musoma District Council
Musoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maji
      • Ujenzi
      • AFYA
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • AFYA
    • KILIMO
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayoanzishwa
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mikataba ya huduma kwa wateja
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

WATAALAM WA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI WAFIKA KUFANYA UFUATILIAJI NA TATHIMINI YA UJENZI WA JENGO LA ONE STOP CENTER

Posted on: January 28th, 2026

Wataalamu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi wamewasili katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kwa lengo la kufanya ufuatiliaji na tathmini ya maendeleo ya ujenzi wa jengo la One Stop Center katika Mwalo wa Busekera, uliopo Kata ya Bukumi.

Kabla ya kuelekea eneo la mradi Busekera, wataalamu hao walipata wasaa wa kukutana na Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Mheshimiwa Juma Chikoka, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Mhe. Maregesi Samweli pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, Ndugu Palela. Katika kikao hicho, viongozi hao walipata fursa ya kubadilishana taarifa kuhusu utekelezaji wa mradi, malengo yake, pamoja na mchango wake katika kuboresha huduma kwa wananchi wa Wilaya ya Musoma.

Ziara hiyo imelenga kukagua hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wa mradi huo, kuhakikisha ujenzi unazingatia viwango, taratibu na michoro iliyopitishwa, pamoja na kutathmini utayari wa kituo hicho katika kurahisisha utoaji wa huduma za sekta ya mifugo na uvuvi.

Ujenzi wa One Stop Center katika Mwalo wa Busekera unatarajiwa kuimarisha usimamizi wa shughuli za uvuvi, kurahisisha huduma kwa wavuvi na wafanyabiashara wa mazao ya uvuvi, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika Kata ya Bukumi na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kwa ujumla.

Halmashauri ya Wilaya ya Musoma itaendelea kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na wadau mbalimbali ili kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na kuleta manufaa yaliyokusudiwa kwa wananchi.

Matangazo

  • MKUTANO WA KWANZA WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI November 27, 2025
  • SIKU YA KUPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI OKTOBA 29, 2025 October 29, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA KATIKA WA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 October 20, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI 2025 October 03, 2025
  • Angalia Yote

Habari za sasa

  • MAFUNZO YA MAANDALIZI YA MPANGO MKAKATI WA SP KWA MIAKA 5 IJAYO KUANZIA 2026/2027–2030/2031

    January 30, 2026
  • WATAALAM WA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI WAFIKA KUFANYA UFUATILIAJI NA TATHIMINI YA UJENZI WA JENGO LA ONE STOP CENTER

    January 28, 2026
  • SIKU YA TATU YA KUTATUA KERO ZA WANANCHI.

    January 28, 2026
  • SIKU YA PILI YA KAMBI MAALUM YA UTATUZI WA KERO ZA WANACHI.

    January 27, 2026
  • Angalia Yote

Video

MANDHARI INAYOPATIKANA KISIWANI RUKUBA, KATA YA ETARO HALMASHAURI YA WILAYA YA MUSOMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal (PEPMIS)
  • Mfumo wa manunuzi (NeST)
  • PREM
  • PReMS
  • GMS
  • Mfumo wa kujisajiri kwa ajili ya bima ya afya (NHIF)

Tovuti mashuhuri

  • OWM - TAMISEMI
  • OR - UTUMISHI
  • NeST
  • NECTA
  • MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Suguti - Kwikonero, Barabara ya Majita) | 31117 - MUSOMA.

    Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma

    Simu: 0282622163

    simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@musomadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa