Wimbo huu wa MLO BORA umetungwa na kuimbwa na wanafunzi wa Klabu ya Lishe ya Shule ya Msingi Nyamrandirira, iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Lengo kuu la wimbo huu ni kuelimisha na kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa lishe bora kwa afya na maendeleo ya watoto.Kupitia wimbo huu, watoto, wazazi na jamii kwa ujumla wanahamasishwa:
Lishe bora ni msingi wa afya njema, akili timamu na maisha bora ya baadaye.Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewahi kusisitiza kuhusu swala la lishe, hasa kwa watoto na akina mama, na kwamba jamii ina wajibu wa kuhakikisha watoto wanapata lishe sahihi ili kujenga taifa lenye afya, nguvu kazi imara na maendeleo endelevu.Tunaamini kuwa elimu kupitia sanaa na muziki hufika kwa urahisi, hugusa hisia za jamii, na huleta *mabadiliko chanya* katika tabia na mtazamo kuhusu lishe bora.
Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, yenye vijiji 68, kata 21 na Tarafa ya Nyanja, ni hazina halisi ya vivutio vya utalii wa ndani—mahali ambapo asili, watu na historia vinakutana kuunda uzoefu usiosahaulika.
Hakikisha unawasha hisia zako za kutafuta uzuri, utulivu na burudani, kwa kutembelea maeneo haya ya kipekee.
Halmashauri ya Wilaya ya Musoma imehitimisha kilele cha maadhimisho ya Lishe Kitaifa katika Kata ya Tegeruka, ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Mhe. Juma Chikoka.
Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Suguti - Kwikonero, Barabara ya Majita) | 31117 - MUSOMA.
Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma
Simu: 0282622163
simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@musomadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa