• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Musoma District Council
Musoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maji
      • Ujenzi
      • AFYA
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • AFYA
    • KILIMO
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayoanzishwa
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mikataba ya huduma kwa wateja
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

Historia

1.0      UTANGULIZI:

Halmashauri ya Wilaya ya Musoma ni moja kati ya Halmashauri tisa (09) za Mkoa wa Mara, ilisimikwa rasmi kama Halmashauri mwaka 1984 chini ya kifungu cha 4 cha sheria za Serikali za Mitaa Sura ya 333.

1.2      ENEO

Halmashauri ya Wilaya ya Musoma ina jumla ya eneo la Kilometa za mraba 2,652.87 (Nchi kavu ni 2,455.87 Km2 na Majini 197 Km2). Umbile la Halmashauri kiujumla ni tambarare likiwa na vilima vidogo vya mtawanyiko.  Halmashauri ipo kusini mashariki mwa ziwa Victoria kati ya nyuzi 1°30’ za Latidudo na Latitudo nyuzi 2°00’ kusini mwa Ikweta Aidha, Halmashauri ipo nyuzi 32°15’na nyuzi 30° Longitudo Mashariki ya mstari wa Grinwichi.

1.2.1   MIPAKA

Halmashauri ya Wilaya ya Musoma inapakana na Manispaa ya Musoma kwa upande wa Kaskazini, Wilaya ya Butiama kwa upande wa Mashariki, Ziwa Victoria upande wa Kusini na Wilaya ya Bunda upande wa kusini mashariki na Ziwa Victoria upande wa Magharibi.

1.2.2   HALI YA HEWA

Halmashauri ipo kwenye mwinuko wa mita 1,500 kutoka usawa wa bahari. Kiwango cha juu cha joto kwa mwaka ni Nyuzi joto kati ya 240C na 320C na kiwango cha chini ni Nyuzi joto kati ya 200C na 240C, kiwango cha mvua ni kati ya 900mm na 1,200mm kwa mwaka, zinazoanza mwezi Oktoba hadi Desemba kwa mvua za vuli na mwezi Machi hadi Mei kwa mvua za masika.

1.3 IDADI YA WATU

Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi iliyofanyika mwezi Agosti mwaka 2022, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma ilikuwa na jumla ya watu 266,665 ambapo kati ya hao, Wanaume ni 131,246 sawa na 49% na Wanawake ni 135,419 sawa na 51%. Ongezeko la watu katika Halmashauri ya wilaya ya Musoma limefikia asilimia 2.1 kutoka mwaka 2012 mpaka 2022. Kwa mujibu wa ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wastani wa pato la Mwananchi kwa mwaka ni Shilingi 2,377,992.01 kwa mwaka.

1.4 HALI YA UCHUMI YA HALMASHAURI YA WILAYA

Shughuli kuu ya kiuchumi kwa wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma ni Uvuvi ambayo huajiri asilimia 85 ya wakazi wote, shughuli nyingine za uchumi ni Kilimo, (5%), Ufugaji (5%), madini (2%) na shughuli nyingine zilizobaki huajiri asilimia 3 ya wakazi. Mazao yanayolimwa ni Alizeti, Ulezi, Muhogo, Mtama na Viazi. Ziada ya Mazao haya ya chakula hutumika kwa biashara. Aidha shughuli za biashara ndogondogo ni ajira mbadala zinazochangia katika pato la wakazi wa Halmashauri ya Musoma.

Matangazo

  • MTIHANI WA KUHITIMU ELIMU YA MSINGI (PSLE) KUANZA SEPTEMBA 10, 2025 NA KUMALIZIKA SEPTEMBA 11, 2025. September 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI 2025 August 29, 2025
  • TANGAZO LA HESABU ZA HALMASHAURI YA WILAYA YA MUSOMA KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 July 01, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 14, 2022
  • Angalia Yote

Habari za sasa

  • WATUMISHI WA UMMA MUSOMA DC WASHIRIKI MAZOEZI YA PAMOJA KUIMARISHA AFYA

    September 13, 2025
  • MTIHANI WA KUHITIMU ELIMU YA MSINGI (PSLE) SEPTEMBA 10 - 11, 2025.

    September 10, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATUA MUSOMA DC

    August 16, 2025
  • WASIMAMIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WAASWA KUZINGATIA SHERIA,MIONGOZO NA TARATIBU ZA UCHAGUZI MKUU 2025

    August 04, 2025
  • Angalia Yote

Video

WATUMISHI WA UMMA MUSOMA DC WASHIRIKI MAZOEZI YA PAMOJA KUIMARISHA AFYA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal (PEPMIS)
  • Mfumo wa manunuzi (NeST)
  • PREM
  • PReMS
  • GMS
  • Mfumo wa kujisajiri kwa ajili ya bima ya afya (NHIF)

Tovuti mashuhuri

  • OR - TAMISEMI
  • OR - UTUMISHI
  • NeST
  • NECTA
  • MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Suguti - Kwikonero, Barabara ya Majita) | 31117 - MUSOMA.

    Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma

    Simu: 0282622163

    simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@musomadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa