Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo Juni 2, 2025 ameshiriki Baraza maalum la madiwani kujadili Hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kwa kupata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo.
Aidha, Mhe. Mtambi ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kwa kufanikiwa kukusanya shilingi bilioni 2.2 za mapato ya ndani hadi tarehe 30 Mei, 2025 na kuitaka kuvuka lengo la makusanyo kwa muda uliobakia.
"Mpaka sasa mmefika asilimia zaidi ya 93 ninauhakika mkijipanga vizuri mtaweza kukusanya zaidi ya asilimia 100" amesema Mtambi.
Mhe. Mtambi ameitaka Halmashauri hiyo kuongeza ubunifu katika kupanua vyanzo vya mapato ya Halmashauri.
Musoma Town opposite to Airport
Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma
Simu: 0282622163
simu ya mkononi:
Barua pepe: ded@musomadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa