• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Musoma District Council
Musoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maji
      • Ujenzi
      • AFYA
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • AFYA
    • KILIMO
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayoanzishwa
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mikataba ya huduma kwa wateja
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

SHULE ZETU NI LAZIMA ZITOE HUDUMA YA CHAKULA

Posted on: November 13th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Ndg.Msongela Palela Leo Novemba 13, 2025 katika ukumbi wa Makanya uliopo Kata ya Mugango Kijiji cha Kwibara amefanya kikao na wakuu wa shule za sekondari na Msingi,Wenyeviti wa vijiji na Vitongoji, Watumishi ngazi ya vijiji na Kata Pamoja na viongozi ngazi ya Halmashauri kwa dhumuni la kuboresha utendaji katika vijiji vyetu hasa utoaji wa elimu bora

“Serikali zetu za vijiji zimejipangaje katika zoezi la utoaji wa chakula shuleni?” Ameuliza Mkurugenzi Msongela ambapo Ndg. Richard Charles ambaye ni mwenyekiti wa Kijiji cha Bulinga amesema sababu kubwa ya wazazi kutochangia chakula cha wanafunzi mashuleni ni matumizi mabaya ya vyakula hivyo kwani vinatumiwa na walimu badala ya wanafunzi na hivyo hawaoni umuhimu wa kuchangia chakula. Sambamba na hilo amesema kuwa ubora wa chakula kinachotolewa shuleni ni mdogo hivyo kupelekea chakula hicho kutoliwa na Watoto wao hivyo hawaoni haja ya kuchangia chakula ambacho Watoto wao hawakitumii

Ndg.Msongela amesisitiza  jamii zetu kushiriki katika utoaji wa chakula shuleni kwani chakula ni hitaji la msingi na sio anasa na mtoto mwenye njaa hawezi kusoma.Tunapochangia chakula, tunachangia  afya,mahudhurio na mafanikio ya wanafunzi wetu.   Ndg. Msongela ameahidi ubora na usalama wa chakula hicho. “Tunaandaa kinyago ambacho kwa kila kata itakayokuwa ya mwisho katika zoezi hili itakichukua na kukaa nacho kwa mwaka mzima ila kwa Kata itakayofanya vizuri nayo itazawadiwa”. Amesisitiza Mkurugenzi

Aidha Utoro shuleni umekithiri katika maeneo yetu. Sisi kama viongozi tunatumia mikakati gani katika kukomesha utoro shuleni?.Kadri tunavyokwenda ndivyo utoro unavyozidi,sasa hawa Watoto wanakwenda wapi? Yawezekana hawa ndio wanaotusumbua huko!

Wakijibu hoja hizo zilizotolewa na Ndg.Palela, wajumbe wa kikao wamesema sababu zinazopelekea utoro shuleni ni Pamoja na mimba za utotoni,uvuvi,ufugaji,uchimbaji madini,mdondoko wa wanafunzi na baadhi ya Watoto kuwa wakuu wa kaya

“Kuanzia leo nawaagiza walimu wakuu na Maafisa elimu Kata kuhakikisha orodha ya watoro inapelekwa kwenye WDC kwa majadiliano. WEO, VEO na Mwenyekiti wa Kijiji wafuatilie kila mwanafunzi mtoro.Kila WEO ahakikishe anawasilisha ofisi ya Mkurugenzi orodha ya wanafunzi waliorejea shuleni wiki ya kwanza ya Januari ,2026 shule zitakapofunguliwa.” Amesisitiza Ndg. Msongela

Aidha, Usalama wa watumishi wanaokuja katika maeneno yetu umeshuka kutokana na  watumishi hasa walimu wakishambuliwa,kuuawa na wengine kuibiwa mali zao. Tunatoa wito kwa serikali za vijiji na Kata kuhakikisha walimu wanalindwa,wanaheshimiwa na wanapata mazingira salama ya kufundishia. “Nakemea tabia ya watumishi wa serikali kuwashambulia Wenyeviti wa Vijiji Pamoja na vitongoji kwani kwa kufanya hivyo ni kuwakosea adabu.sisi ni wamoja hivyo inabidi tufanye kazi kwa kushirikiana” . Amesisitiza Mkurugenzi Palela

Ndg. Palela amesisitiza Uandikishaji wa wanafunzi wa kidato cha kwanza,MEMKWA, darasa la kwanza na awali kwa mwaka 2026 uanze mara moja. Ifikapo Desemba 31,2025 uandikishaji uwe umekamilika ili wanafunzi waanze masomo kwa wakati. Wenyeviti tuna jukumu la kuhakikisha Watoto wetu wote wanaandikishwa kutokana na changamoto ya jamii tuliyonayo kwa wazazi kutoridhia Watoto wao waende shuleni. Wanafunzi wote lazima waandikishwe na kuhudhulia shuleni haijalishi kama ana sare ya shule au hana ili tupate ufumbuzi wake. Lazima sisi wenyeviti tuunge mkono serikali yetu kwa kuhakikisha wanafunzi wote wanaenda shule

Naomba taarifa tunazotoa kutoka katika maeneo yetu ziwe sahihi na za kweli kwani kumekuwa na tabia ya kutoa taarifa zisizo za kweli na kupelekea kufanya maamuzi yasiyo sahihi katika maeneo yetu kutokana na taarifa hizo.Pia tuangalie namna ya kutenga maeneo yetu kwa ajili ya shughuli mbalimbali za miradi ya serikali kama ujenzi wa shule Pamoja na Zahanati.Fedha za miradi zinapoletwa na serikali katika maeneo yetu ila sisi watendaji kwa ngazi ya vijiji tunaendelea kuvutana kuhusu maeneo ya miradi hii. Ni lazima tufanye maamuzi sasa ya kutenga maeneo ya miradi ili kujilidhisha na maeneo hayo na kama itawezekana kuyatafutia hati miliki ili kuondoa migogoro inayoweza kujitokeza

Matangazo

  • SIKU YA KUPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI OKTOBA 29, 2025 October 29, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA KATIKA WA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 October 20, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI 2025 October 03, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 14, 2022
  • Angalia Yote

Habari za sasa

  • SHULE ZETU NI LAZIMA ZITOE HUDUMA YA CHAKULA

    November 13, 2025
  • WANANCHI WA KIJIJI CHA KATARYO KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA LISHE KITAIFA 2025

    November 21, 2025
  • KILELE CHA MAADHIMISHO YA LISHE KITAIFA KATIKA KIJIJI CHA KATARYO KILICHOPO KATA YA TEGERUKA.

    November 21, 2025
  • KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI YAANZA TATHMINI YA MAOMBI YA MIKOPO YA TSH 700 MILIONI KWA VIKUNDI VYA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    November 19, 2025
  • Angalia Yote

Video

KILELE CHA MAADHIMISHO YA LISHE KITAIFA YALIYOFANYIKA KIJIJI CHA KATARYO KATA YA TEGERUKA 2025
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal (PEPMIS)
  • Mfumo wa manunuzi (NeST)
  • PREM
  • PReMS
  • GMS
  • Mfumo wa kujisajiri kwa ajili ya bima ya afya (NHIF)

Tovuti mashuhuri

  • OWM - TAMISEMI
  • OR - UTUMISHI
  • NeST
  • NECTA
  • MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Suguti - Kwikonero, Barabara ya Majita) | 31117 - MUSOMA.

    Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma

    Simu: 0282622163

    simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@musomadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa