• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Musoma District Council
Musoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maji
      • Ujenzi
      • AFYA
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • AFYA
    • KILIMO
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayoanzishwa
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mikataba ya huduma kwa wateja
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

WATAALAMU WAKAMILISHA TATHMINI YA AWALI YA UJENZI WA ONE STOP CENTER MWALO WA BUSEKERA

Posted on: February 1st, 2026

Wataalamu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, wamekamilisha zoezi la tathmini ya awali ya eneo lote pamoja na mapitio ya michoro ya awali inayoonesha mpangilio wa soko na majengo yatakayojengwa katika Mwalo wa Busekera, eneo linalotarajiwa kuanza ujenzi wa One Stop Center.

Baada ya kukamilika kwa tathmini hiyo, wataalamu hao walifanya kikao maalum na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, Ndugu Msongela Nitu Palela, ambaye alipokea rasmi taarifa ya awali ya mwenendo mzima wa mradi kwa niaba ya Menejimenti ya Halmashauri.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, Ndugu Palela, aliwashukuru kwa dhati wataalamu hao kwa ujio wao, ushirikiano waliouonesha, pamoja na hatua za awali walizochukua katika kutathmini eneo na michoro ya mradi huo muhimu, hatua ambazo zimeweka msingi mzuri wa utekelezaji wa ujenzi wa One Stop Center katika Mwalo wa Busekera.

Ilielezwa pia kuwa taarifa hiyo ni ripoti ya awali inayotoa mwelekeo wa jumla wa utekelezaji wa mradi, ikiwemo hatua zilizofikiwa, maandalizi yaliyokamilika, pamoja na mapendekezo ya kitaalamu kabla ya kuanza rasmi kwa hatua za ujenzi.

Halmashauri ya Wilaya ya Musoma itaendelea kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na wadau wengine ili kuhakikisha mradi huo unatekelezwa kwa ufanisi, kwa kuzingatia taratibu, viwango na ratiba zilizopangwa, kwa manufaa ya wananchi na maendeleo ya sekta ya mifugo na uvuvi.

Matangazo

  • MKUTANO WA KWANZA WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI November 27, 2025
  • SIKU YA KUPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI OKTOBA 29, 2025 October 29, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA KATIKA WA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 October 20, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI 2025 October 03, 2025
  • Angalia Yote

Habari za sasa

  • Programu ya Utoaji wa Chakula Shuleni – Shule ya Msingi Nyaminya B.

    February 06, 2026
  • KUGUNDULIWA KWA MGODI MPYA KIJIJI CHA MABUIMERAFURU - KATA YA MUSANJA KUNAFUNGUA FURSA ZA AJIRA, UKWAMUAJI WA KIUCHUMI NA KUONGEZA MAPATO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA MUSOMA

    February 05, 2026
  • WATAALAMU WAKAMILISHA TATHMINI YA AWALI YA UJENZI WA ONE STOP CENTER MWALO WA BUSEKERA

    February 01, 2026
  • MAFUNZO YA MAANDALIZI YA MPANGO MKAKATI WA SP KWA MIAKA 5 IJAYO KUANZIA 2026/2027–2030/2031

    January 30, 2026
  • Angalia Yote

Video

KLABU YA LISHE YA SHULE YA MSINGI NYAMRANDIRIRA || MLO BORA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal (PEPMIS)
  • Mfumo wa manunuzi (NeST)
  • PREM
  • PReMS
  • GMS
  • Mfumo wa kujisajiri kwa ajili ya bima ya afya (NHIF)

Tovuti mashuhuri

  • OWM - TAMISEMI
  • OR - UTUMISHI
  • NeST
  • NECTA
  • MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Suguti - Kwikonero, Barabara ya Majita) | 31117 - MUSOMA.

    Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma

    Simu: 0282622163

    simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@musomadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa