• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Musoma District Council
Musoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maji
      • Ujenzi
      • AFYA
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • AFYA
    • KILIMO
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayoanzishwa
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mikataba ya huduma kwa wateja
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

MUSOMA DC YATOA MILIONI 135.4 MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA VIKUNDI 11 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU

Posted on: January 9th, 2026

Halmashauri ya Wilaya ya Musoma imetoa jumla ya shilingi milioni 135,420,000 kwa ajili ya mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi 11, ikihusisha vikundi 05 vya wanawake, 03 vya vijana na 03 vya watu wenye ulemavu, katika mwaka wa fedha 2025/2026, ikiwa ni awamu ya kwanza ya utoaji wa mikopo hiyo.

Akizungumza katika hafla ya utoaji wa mikopo isiyo na riba iliyofanyika tarehe 09 Januari, 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Charles Magoma, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, Ndugu Majidu Mudrikat Kalugendo, amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amekuwa sauti na nguzo kubwa katika kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia mikopo isiyo na riba inayotolewa na Halmashauri kwa mujibu wa sheria.

Kalugendo amesema kuwa jukumu kubwa kwa sasa ni kurahisisha utoaji wa mikopo hiyo na kuhakikisha waombaji hawapati changamoto, huku Halmashauri ikijipanga kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna bora ya kuunda vikundi, kuomba mikopo, pamoja na kuhakikisha urejeshaji unafanyika kwa ufanisi.

“Hatua hizi ni sehemu ya kuhakikisha tunatimiza dhamira ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia mikopo ya asilimia 10 inayotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri,” amesisitiza Kalugendo.

Aidha, amewatoa hofu wananchi kuhusu upatikanaji wa mikopo hiyo kwa kusisitiza kuwa fedha zipo na zitawafikia wanufaika wote waliokidhi vigezo, ambapo mikopo hiyo inatarajiwa kuchangia kuongeza kipato cha familia na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.

 Mikopo hiyo itatolewa kupitia mfumo wa kibenki, ambapo Benki ya NMB na Benki ya CRDB zimepewa jukumu la kusimamia utoaji wa fedha kwa vikundi vilivyoidhinishwa. Mfumo huu unalenga kuhakikisha uwazi, usalama wa fedha, pamoja na ufuatiliaji mzuri wa urejeshaji wa mikopo.

Matangazo

  • MKUTANO WA KWANZA WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI November 27, 2025
  • SIKU YA KUPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI OKTOBA 29, 2025 October 29, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA KATIKA WA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 October 20, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI 2025 October 03, 2025
  • Angalia Yote

Habari za sasa

  • MUSOMA DC YATOA MILIONI 135.4 MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA VIKUNDI 11 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU

    January 09, 2026
  • KAMATI YA MAAFA YA WATAALAM KUTOKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MUSOMA IMEFANYA TATHMINI YA ATHARI ZA MVUA KUBWA KIJIJI CHA KURWAKI.

    December 31, 2025
  • ZIARA YA MGUU KWA MGUU YA MKUU WA WILAYA YA MUSOMA, MHE. JUMA CHIKOKA, PAMOJA NA TIMU YA MENEJIMENTI

    December 30, 2025
  • DKT. BASHIRU AALIKA WAWEKEZAJI WA NDANI KUCHANGAMKIA UFUGAJI WA SAMAKI KWA NJIA YA VIZIMBA

    December 22, 2025
  • Angalia Yote

Video

MANDHARI INAYOPATIKANA KISIWANI RUKUBA, KATA YA ETARO HALMASHAURI YA WILAYA YA MUSOMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal (PEPMIS)
  • Mfumo wa manunuzi (NeST)
  • PREM
  • PReMS
  • GMS
  • Mfumo wa kujisajiri kwa ajili ya bima ya afya (NHIF)

Tovuti mashuhuri

  • OWM - TAMISEMI
  • OR - UTUMISHI
  • NeST
  • NECTA
  • MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Suguti - Kwikonero, Barabara ya Majita) | 31117 - MUSOMA.

    Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma

    Simu: 0282622163

    simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@musomadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa