• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Musoma District Council
Musoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maji
      • Ujenzi
      • AFYA
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • AFYA
    • KILIMO
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayoanzishwa
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mikataba ya huduma kwa wateja
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

MVUA YASABABISHA MAAFA KIJIJI CHA KAMGURUKI PAMOJA NA KABEGI

Posted on: February 7th, 2024

Mwenyekiti wa Maafa Wilaya ya Musoma Mhe. Dkt. Khalifany Haule akiambatana na Kamati ya usalama Wilaya pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya Ndg. Majidu Kalugendo Leo Februari 7, 2024 wamewatembelea wanakijiji wa Kijiji Cha Kabegi pamoja na Kamguruki kwa ajili ya kuwapa pole na kutoa msaada wa chakula (Mahindi na Maharage) vitakavyowasaidia katika kipindi hiki kigumu baada ya kukumbwa na Maafa yaliyoletwa na Mvua kubwa iliyoambatana na upepo iliyonyesha Usiku wa kuamkia Tarehe 5, Februari 2024.


Jumla ya Nyumba 17 zimeezuliwa paa na Nyumba 2 kubomoka katika Kijiji Cha Kabegi.Katika Kijiji Cha Kamguruki Nyumba 3 zimeezuliwa paa na Nyumba 1 kubomoka Kuta na kusababisha Kifo Cha mtoto wa Miezi 9 aitwae Wambura Dickson Wambura.


Mwenyekiti wa Kijiji Cha kabegi Ndg. Charles Choto amemshukuru Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dkt. Khalifany Kwa kuwa bega Kwa bega na Wananchi wa Vijiji hivi kwani amekuwa nao tangu Tarehe 5 majanga haya yalipotokea Kwa ulinzi pamoja na huduma muhimu za kijamii Kwa waliofikwa na janga hili.


Pia Mwenyekiti wa Kijiji Cha kamguruki Ndg. Alvin Wanzagi Amemshukuru pia Mhe. Mkuu wa Wilaya Kwa kuwagusa Wananchi katika kijiji chake kilichoathirika. "Serikali ya Mhe.Rais  Dkt. Samia Suluhu Hassan haijawahi kuwa nyuma  katika kuwasaidia Wananchi wake" Amesisitiza Ndg.Alvin.


Diwani wa Kata ya Nyakatende Mhe. Gerald Mfungo Kasonyi Ameishukuru  Serikali ya awamu hii Kwa kuwajali Wananchi wake na kuahidi kufanya kazi bega Kwa bega na Serikali Kwa juhudi zake za kusaidia wananchi . Mhe. Kasonyi ametoa mchango wake wa Sabuni Kwa familia zote zilizokumbwa na janga hili na kuahidi kuwa sambamba katika uimarishaji wa makazi ya wahanga wa Vijiji hivi.


Dkt. Haule amewashukuru Wenyeviti wa Vijiji hivi pamoja na wakazi wa Vijiji hivi Kwa kuonesha Moyo wa upendo wa  kuwasaidia Wananchi waliopata majanga haya pia Kwa michango yao waliyochanga Tshs 200,000/= Kwa ajili ya kusaidia Kaya zilizoathirika. "Pia naishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Kwa michango yake kwenye Vijiji hivi Ili kuwasaidia waliokumbwa na janga hili " Dkt. Haule akishukuru .

Matangazo

  • SIKU YA KUPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI OKTOBA 29, 2025 October 29, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA KATIKA WA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 October 20, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI 2025 October 03, 2025
  • WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023 December 14, 2022
  • Angalia Yote

Habari za sasa

  • WANANCHI WA KIJIJI CHA KATARYO KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA LISHE KITAIFA 2025

    November 21, 2025
  • KILELE CHA MAADHIMISHO YA LISHE KITAIFA KATIKA KIJIJI CHA KATARYO KILICHOPO KATA YA TEGERUKA.

    November 21, 2025
  • KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA HALMASHAURI YAANZA TATHMINI YA MAOMBI YA MIKOPO YA TSH 700 MILIONI KWA VIKUNDI VYA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    November 19, 2025
  • SALAMU ZA PONGEZI KUTEULIWA KUWA WAZIRI MKUU WA TANZANIA 2025 - 2030

    November 18, 2025
  • Angalia Yote

Video

KILELE CHA MAADHIMISHO YA LISHE KITAIFA YALIYOFANYIKA KIJIJI CHA KATARYO KATA YA TEGERUKA 2025
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal (PEPMIS)
  • Mfumo wa manunuzi (NeST)
  • PREM
  • PReMS
  • GMS
  • Mfumo wa kujisajiri kwa ajili ya bima ya afya (NHIF)

Tovuti mashuhuri

  • OWM - TAMISEMI
  • OR - UTUMISHI
  • NeST
  • NECTA
  • MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Suguti - Kwikonero, Barabara ya Majita) | 31117 - MUSOMA.

    Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma

    Simu: 0282622163

    simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@musomadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa