• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Musoma District Council
Musoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maji
      • Ujenzi
      • AFYA
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • AFYA
    • KILIMO
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayoanzishwa
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mikataba ya huduma kwa wateja
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

TARATIBU ZA UTOAJI MIKOPO ZIHESHIMIWE

Posted on: March 14th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilayaya Musoma Ndg. Msongela Palela, amewataka Wananchi  kutumia mikopo wanayokopa kufanya uwekezaji unaozalisha faida ilikuepuka kushindwa kufanya marejesho ya mikopo hiyo. Ndg. Palela alitoa rai hiyo wakati alipokutana na Timu ya Wataalamu kutoka Wizara ya Fedha, Taasisi za Serikali na Binafsi ambayo ipo Mkoani Mara kutoa elimu ya fedha kwa makundi mbalimbali. "Kwenye Wilaya yetu kumekuwa na changamoto kwa Wananchi wetu kuchukua mikopo na hawaendi kuwekeza kwenye maeneo ambayo yatazalisha faida ili watumie faida ile kufanya marejesho", alisema Ndg. Palela.

Aliongeza kuwa wananchi kukopa sio jambo baya lakini alitarajia mikopo hiyo iwasaidie lakini imekua tofauti kwasababu haiendi kutumiwa katika shughuli za uzalishaji hivyo wanashindwa kufanya marejesho Ndg. Palela alifafanua kuwa elimu ya fedha ni muhimu hivyo ni vyema Wizara ya Fedha ikahakikisha inawafikia Wananchi wote na elimu hiyo iwe endelevu kwakuwa inamchango mkubwa katika kuchangia uchumi wa nchi endapo itaeleweka kwa wananchi wote.

Aidha, alizitaka Taasisi za Fedha zinazojihusisha na utoaji mikopo, kufuata utaratibu na Sheria zilizowekwa na Serikali ili mikopo wanayotoa kwa wananchi iwasaidie na isiwe chanzo cha kuongeza tatizo kwa kuweka riba kubwa zisizolipika kwa urahisi. "Naendelea kuwaomba watoa huduma za fedha kuwa waaminifu na kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu zilizowekwa na Benki Kuu ya Tanzania za kuwalinda watoa huduma na wateja. Vilevile, aliwataka Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kujenga utaratibu wa kutumia Taasisi rasmi zinazotambuliwa na Serikali wanapohitaji mikopo, ilikuepuka udhalilishaji unaofanywa na Taasisi ambazo haziko rasmi na hazifuati utaratibu.

Ndg. Palela aliipongeza Wizara ya Fedha kwa kushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa kuendelea kuwachukulia hatua watoa huduma wanaofanyabiashara kinyume na utaratibu unavyoelekeza Naye mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo Bw. Mbagira Kajanja, aliishukuru Serikali kwa kuwapatia elimu ya fedha ambapo alieleza kupitia elimu hiyo imewafumbua macho na kuelewa baadhi ya taratibu ikiwemo kuwa na haki ya kusoma mkataba kabla ya kuchukua mkopo.

Matangazo

  • SIKU YA KUPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI OKTOBA 29, 2025 October 29, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI 2025 October 03, 2025
  • MTIHANI WA KUHITIMU ELIMU YA MSINGI (PSLE) KUANZA SEPTEMBA 10, 2025 NA KUMALIZIKA SEPTEMBA 11, 2025. September 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI 2025 August 29, 2025
  • Angalia Yote

Habari za sasa

  • MHE. MTAMBI AWATAKA WAJASIRIAMALI WA MARA KUREJESHA MIKOPO KWA WAKATI NA KUSHIRIKI UCHAGUZI 2025

    October 02, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA MUSOMA MHE JUMA ISSA CHIKOKA ASHIRIKI MUSOMA BONANZA ILIYOAMBATANA NA SHUGHULI MBALIMBALI

    September 27, 2025
  • KILIMO CHA BUSTANI KWA TEKNOLOJIA YA UMWAGILIAJI WA MATONE (DRIP IRRIGATION SYSTEM) SHULE YA MSINGI NYETASYO

    September 25, 2025
  • WATUMISHI AJIRA MPYA 149 KUTOKA DIVISHENI NA VITENGO MBALIMBALI WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI.

    September 18, 2025
  • Angalia Yote

Video

WATUMISHI WA UMMA MUSOMA DC WASHIRIKI MAZOEZI YA PAMOJA KUIMARISHA AFYA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal (PEPMIS)
  • Mfumo wa manunuzi (NeST)
  • PREM
  • PReMS
  • GMS
  • Mfumo wa kujisajiri kwa ajili ya bima ya afya (NHIF)

Tovuti mashuhuri

  • OR - TAMISEMI
  • OR - UTUMISHI
  • NeST
  • NECTA
  • MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Suguti - Kwikonero, Barabara ya Majita) | 31117 - MUSOMA.

    Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma

    Simu: 0282622163

    simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@musomadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa