• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Musoma District Council
Musoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maji
      • Ujenzi
      • AFYA
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • AFYA
    • KILIMO
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayoanzishwa
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mikataba ya huduma kwa wateja
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

WAWEKEZAJI WA NDANI KUCHANGAMKIA UFUGAJI WA SAMAKI KWA NJIA YA VIZIMBA.

Thursday 8th, January 2026
@KIJIJI CHA SUGUTI NA KIJIJI CHA BUSEKERA

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amewataka wawekezaji wa ndani kuchangamkia fursa nyingi zilizopo katika tasnia ya ufugaji wa samaki nchini, hususan ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba.

Balozi Dkt. Bashiru ametoa wito huo Desemba 22, 2025, wakati wa ziara yake Wilayani Musoma katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, ambapo alifika Kijiji cha Suguti, Kata ya Suguti, kukutana na wafugaji wa samaki kwa njia ya vizimba kwa lengo la kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili katika shughuli zao za ufugaji.

Akiwa Suguti, Waziri amehimiza wawekezaji wa ndani kuelekeza nguvu zao katika uanzishaji wa viwanda vya chakula cha samaki, uzalishaji wa vifaranga vya samaki pamoja na utoaji wa mikopo kwa vikundi vinavyojihusisha na ufugaji wa samaki, akisisitiza kuwa sekta hiyo ina tija kubwa kiuchumi.

“Ufugaji wa samaki ni utajiri. Pamoja na changamoto zilizopo, wafugaji wengi wanaendelea na shughuli hii kwa sababu ya faida inayopatikana. Tunawakaribisha wawekezaji wa ndani hususan katika eneo la uzalishaji wa vifaranga ili kuhakikisha vinapatikana kwa wakati wote,” amesema Balozi Dkt. Bashiru.

Baada ya hapo, Waziri alitembelea wavuvi wa samaki katika Kijiji cha Busekela, Kata ya Bukumi, ambapo alisikiliza changamoto zinazowakabili wavuvi hao na kuahidi Serikali kuendelea kuboresha mazingira ya uvuvi ili kuongeza tija na kipato kwa wananchi.

Aidha, Balozi Dkt. Bashiru amesisitiza kuwa tasnia ya ufugaji wa samaki ni miongoni mwa maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yaliyolenga kuwawezesha wanawake na vijana kiuchumi kupitia sekta ya uvuvi, hivyo amewahimiza wananchi kuchangamkia fursa zilizopo.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Ng’wasi Kamani, amesema wanawake na vijana wanaojihusisha na ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba wameanza kunufaika na programu hiyo, huku Serikali ikiendelea kushughulikia changamoto zinazojitokeza. Mmoja wa wanufaika amesema wafugaji waliopata mikopo ya vizimba awamu ya kwanza waliweza kuvuna samaki wengi na kurejesha mikopo yao licha ya changamoto za awali na Ziara hiyo imeendelea Wilayani Bunda

Matangazo

  • MKUTANO WA KWANZA WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI November 27, 2025
  • SIKU YA KUPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI OKTOBA 29, 2025 October 29, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE SEMINA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA KATIKA WA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 October 20, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI 2025 October 03, 2025
  • Angalia Yote

Habari za sasa

  • KAMATI YA MAAFA YA WATAALAM KUTOKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MUSOMA IMEFANYA TATHMINI YA ATHARI ZA MVUA KUBWA KIJIJI CHA KURWAKI.

    December 31, 2025
  • ZIARA YA MGUU KWA MGUU YA MKUU WA WILAYA YA MUSOMA, MHE. JUMA CHIKOKA, PAMOJA NA TIMU YA MENEJIMENTI

    December 30, 2025
  • DKT. BASHIRU AALIKA WAWEKEZAJI WA NDANI KUCHANGAMKIA UFUGAJI WA SAMAKI KWA NJIA YA VIZIMBA

    December 22, 2025
  • ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUCHAGUA ENEO LA UJENZI WA STENDI.

    December 19, 2025
  • Angalia Yote

Video

MANDHARI INAYOPATIKANA KISIWANI RUKUBA, KATA YA ETARO HALMASHAURI YA WILAYA YA MUSOMA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal (PEPMIS)
  • Mfumo wa manunuzi (NeST)
  • PREM
  • PReMS
  • GMS
  • Mfumo wa kujisajiri kwa ajili ya bima ya afya (NHIF)

Tovuti mashuhuri

  • OWM - TAMISEMI
  • OR - UTUMISHI
  • NeST
  • NECTA
  • MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Suguti - Kwikonero, Barabara ya Majita) | 31117 - MUSOMA.

    Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma

    Simu: 0282622163

    simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@musomadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa