• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Musoma District Council
Musoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Maji
      • Ujenzi
      • AFYA
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • AFYA
    • KILIMO
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi itakayoanzishwa
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Mpango Mkakati
    • Mikataba ya huduma kwa wateja
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi

VIJIJI 31 MUSOMA DC KUNUFAIKA NA MRADI WA SERIKALI WA MAJI SAFI NA SALAMA (WSDP)

Posted on: September 17th, 2018


Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kwa kushirikiana na serikali kupitia Wizara ya maji na umwagiliaji imeanza  mpango wa kupeleka maji katika vijiji 31 vinavyozungukwa na Ziwa Victoria, vilivyopo katika Halmashauri hiyo.


Vijiji vitakavyonufaika na mradi huo ni Busekera, Buira na Bukumi vilivyopo Kata ya Bukumi, Kastam Kata ya Bukima, Buanga na Rusoli Kata ya Rusoli, Musanja Kata ya Musanja, Bugwema, Masinono na Kinyang'erere Kata ya Bugwema, Murangi na Lyasembe Kata ya Murangi, Kasoma, Chumwi na Kaboni Kata ya Nyamrandirira, Tegeruka Kata ya Tegeruka, Maneke, Mwiringo na Kwikuba Kata ya Busambara, Kiriba, Bwai Kwitururu na Bwai Kumsoma Kata ya Kiriba, Kiemba na Kabegi Kata ya Ifulifu, Kigera Etuma/ Kakisheri Kata ya Nyakatende, Kurukerege na Mkirira Kata ya Nyegina, Kisiwa cha Rukuba, Mmahare, Busamba na Etaro Kata ya Etaro,


Mradi  huo wa serikali wa kusambaza maji katika vijiji vinavyozunguka katika maziwa makuu ambayo ni Ziwa Victoria, Tanganyika na Rukwa umeingia katika awamu ya pili baada ya  awamu ya kwanza mwaka 2006 - 2015.


Mradi huo unaojulikana kwa jina là Programu ya uendelezaji wa sekta ya Maji awamu ya pili (WSDP II) umepangwa kuzunguka katika Mikoa mitano, Wilaya 19 na Vijiji 271.


Mikoa itakayonufaika na mradi huo ni Mara, Mwanza, Kagera, Simiyu na Geita.


Akizungumza wakati wa kikao kati ya wataalamu wa maji na wananchi wa kijiji cha Bwai Kwitururu kilichopo Kata ya Kiriba, mtaalamu wa Maji kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji Mhandisi Grayson Mdemu alisema mradi huo hakuna mwanakiji atakayelipwa fidia kwa kuwa mradi huo hautobomoa Nyumba ya mtu.


"Mradi huu utagharamiwa kwa asilimia 100 na Serikali   ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hakuna mwananchi atakayelipwa fidia kutokana na mabomba kupita katika maeneo yenu, kwa kuwa hatutobomoa nyumba ya mtu yoyote kupitisha mabomba hayo" alisema Mhandisi Mdemu.


"Mradi huu una faida kuu tatu kuleta maji safi na salama kwa wananchi (Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya Mwaka 2015 -  2020 ibara ya 55 kipengele A, kuboresha afya za wananchi na kuinua hali za uchumi" .


Wakati huo Mhandisi wa Maji Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Mhandisi Emmanuel Masanja aliwataka wananchi wa vijiji hivyo 31 kuutunza na kuulinda mradi huo kipindi utakapoanza.


"Serikali imeamua kutuletea mradi wa maji katika vijiji 31 vilivyopo katika Halmashauri yetu, hii ni bahati na inatupasa kuulinda na kuutunza utakapoanza mradi huo " alisema Mhandisi Masanja.


Imetolewa na

Kitengo cha Habari na Uhusiano

Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

Matangazo

  • SIKU YA KUPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI OKTOBA 29, 2025 October 29, 2025
  • MTIHANI WA KUHITIMU ELIMU YA MSINGI (PSLE) KUANZA SEPTEMBA 10, 2025 NA KUMALIZIKA SEPTEMBA 11, 2025. September 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI 2025 August 29, 2025
  • TANGAZO LA HESABU ZA HALMASHAURI YA WILAYA YA MUSOMA KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 July 01, 2025
  • Angalia Yote

Habari za sasa

  • MKUU WA MKOA WA MARA MHE. KANALI EVANS ALFRED MTAMBI AMKABIDHI MKURUGENZI MTENDAJI (W) NDUGU. MSONGELA NITU PALELA CHETI CHA KUTHAMINI (CERTIFICATE OF APPRECIATION) KWENYE MAADHIMISHO YA KILELE CHA MARA DAY YALIYOFANYIKA WILAYANI BUTIAMA 15 SEPTEMBA 2025.

    September 15, 2025
  • WATUMISHI WA UMMA MUSOMA DC WASHIRIKI MAZOEZI YA PAMOJA KUIMARISHA AFYA

    September 13, 2025
  • MTIHANI WA KUHITIMU ELIMU YA MSINGI (PSLE) SEPTEMBA 10 - 11, 2025.

    September 10, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WATUA MUSOMA DC

    August 16, 2025
  • Angalia Yote

Video

WATUMISHI WA UMMA MUSOMA DC WASHIRIKI MAZOEZI YA PAMOJA KUIMARISHA AFYA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Watumishi Portal (PEPMIS)
  • Mfumo wa manunuzi (NeST)
  • PREM
  • PReMS
  • GMS
  • Mfumo wa kujisajiri kwa ajili ya bima ya afya (NHIF)

Tovuti mashuhuri

  • OR - TAMISEMI
  • OR - UTUMISHI
  • NeST
  • NECTA
  • MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO (e-GA)
  • AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (Suguti - Kwikonero, Barabara ya Majita) | 31117 - MUSOMA.

    Sanduku la Posta: P.o. Box 344 Musoma

    Simu: 0282622163

    simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@musomadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Malalamiko
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Sitemap
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Haki zote zimehifadhiwa